
Siku chache zilizopita Justin Bieber alitangaza ujio wa album yake mpya ‘Purpose’kupitia page yake ya Twitter. Kwa sasa msanii huyo mwenye miaka 21 anaendelea kuweka headlines kwenye chati mbalimbali za duniani ikiwemo chati ya Billboard Hot 100 ambapo single yake mpya ya ‘What Do You Mean‘ imeendelea kushikilia nafasi ya kwanza kwa wiki kadhaa sasa.
Wakati tukiwa tunaendelea kusibira ujio wa album hiyo, cover ya Album mpya ya Justin Bieber imeshaanza kusambaa mitandaoni… album hiyo mpya itaanza kupatikana kuanzia tarehe 13 November 2015 ikiwa imebeba hit single yake mpya ‘What Do You Mean’.
Kingine kizuri kuhusu album hii ni kwamba, Justin Bieber safari hii kafanya kazi na wasanii wa kubwa kwenye muziki wa Hip Hop kama Kanye West, kafanya kazi pia na Dj Skrillex ambae alishawahi kufanya nae kazi kwenye single yake ya ‘Where Are U Now’.
No comments :