
Kila siku asubuhi huwa nazisogeza headlines zilizobebwa kwenye kurasa za Magazeti ya Tanzania, Uchambuzi wa stori zote napandisha kwenye account yangu ya Twitter>>>@millardayo na Zote nakusogezea hapa chini.
Moja ya stori kubwa ni hii ya gazeti la Mtanzania yenye kichwa cha habari ‘Wanaume wenye korodani zisizoshuka hatarini’, Gazeti
hilo limeripoti kuwa wanaume ambao korodani zao hazijashuka kwenye
mfuko wake wapo hatarini kwani kuna uwezekano mkubwa wa kugeuka kuwa
saratani zikiwa tumboni.
Gazeti hilo lilifanya mahojiano na Daktari Bingwa wa Mfumo wa Njia ya Mkojo wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ‘MNH’ Ryuba Nyamsogoro ambapo aliyazungumza haya………
>>>’kawaida
mwanaume ana korodani mbili, moja ikiwa upande wa kushoto na nyingine
upande wake wa kulia. Huwa zinatengenezewa tumboni na baadae hushuka
hadi katika vifuko vyake vilivyoko nje ya mwili wa mwanaume karibu na
uume‘
Daktari
alieleza sababu mbalimbali ambazo huweza kuchangia hali hiyo ikiwamo
mtoto kuzaliwa akiwa hajatimiza muda wake (njiti), pacha au kuzaliwa
akiwa na upungufu wa homoni ya androgen.
Daktari
huyo aliongeza kuwa tafiti zinaonyesha kuwa katika vizazi hai 100 vya
watoto wa kiume kila mwaka ulimwenguni wanne huzaliwa wakiwa na tatizo
hilo.
>>>’Kwa
hapa nchini bado hatuna takwimu halisi za hali ilivyo lakini hapa
muhimbili tumekua tukipokea takribani watoto wanne wenye tatizo la
korodani kutoshuka na kuwafanyia upasuaji’ :- Daktari
No comments :